Daktari
 kijana Brian Mushi wa Projeckt Inspire akionyesha upendo kwa mmoja wa 
wazee wanaoishi kwenye kituo hicho kilichopo Msimbazi Centre mara baada 
ya kumpima Presha wakati wa maadhimisho ya siku ya wazee duniani.
Na Mwandisi wetu
WAZEE
 wanaoshi katika makazi ya Msimbazi Centre Jijini Dar es salaam karibu 
na kanisa la Mtakatifu Maria wa Fatma, Msimbazi walipata faraja kubwa 
baada ya kutembelewa na makundi matatu ya jamii.
Makundi
 hayo ni pamoja na wafanyakazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa 
linaloshughulikia Idadi ya watu duniani (UNFPA) hapa nchini, Tushikamane
 Pamoja Foundation na madaktari vijana wanaounda kundi la Projeckt 
Inspire chini ya mradi wa Inspire Healthy.
Makundi hayo yalifika katika kituo hicho katika kuadhimisha siku ya wazee duniani.
Wakiwa
 na lengo kuu la kuwafariji, kukagua afya zao na kuheshimu uwepo wao, 
makundi hayo pia yaliwapa zawadi za  vyandarua, sabuni za kufulia na 
kuogea, pampers, Thermos Flask, vikombe vya chai, sahani za kulia, 
vijiko, sukari, njugu mawe, Tshirts, viatu, nguo, vyombo vya kufanyia 
usafi .
Pia walipiga picha za pamoja za ukumbusho.
Siku ya Wazee Duniani imetengwa kwa ajili ya kuweaenzi na pia kuwakumbuka kwa mambo waliyofanya kuendeleza kizazi cha wanadamu.
Dr. Brian Mushi wa Projeckt Inspire akimpima presha mmoja wa wazee wanaoishi kwenye kituo hicho.
Dr.
 Brian Mushi wa Projeckt Inspire akichukua vipimo vya damu kwa ajili ya 
kupima sukari kwa mmoja wa wazee wanaolelewa kwenye kituo hicho wakati 
wa maadhimisho ya siku ya wazee duniani.
Wafanyakazi
 wa UNFPA kutoka kushoto ni Clementina Njau, Mike Mwakuvila na mdau 
kutoka Tushikamane Pamoja Foundation wakionyesha upendo kwa mmoja wa 
wazeee wanaoishi kwenye kituo hicho wakati wa maadhimisho ya siku ya 
wazee duniani.
Dr.
 Majaliwa Marwa kutoka UNFPA akikabidhi moja ya vyandarua walivyovitoa 
kwenye kituo hicho kinacholelea wazee Msimbazi Centre wakati wa 
maadhimisho ya siku ya wazee duniani.
Sehemu ya msaada uliotolewa na makundi hayo.
Wafanyakazi
 wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu duniani 
(UNFPA) hapa nchini wakiongozwa na mtaalam wa mawasiliano kutoka UNFPA, 
Sawiche Wamunza(kushoto), wadau wa Tushikamane Pamoja Foundation pamoja 
madaktari vijana wanaounda kundi la Projeckt Inspire chini ya mradi wa 
Inspire Healthy wakiwa kwenye picha ya pamoja na masista wanaowahudumia 
wazee hao kwenye kituo hicho.
Wafanyakazi
 wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu duniani 
(UNFPA) hapa nchini wakiongozwa na mtaalam wa mawasiliano kutoka UNFPA, 
Sawiche Wamunza(wa nne kushoto), wadau wa Tushikamane Pamoja Foundation 
pamoja madaktari vijana wanaounda kundi la Projeckt Inspire chini ya 
mradi wa Inspire Healthy kwenye picha ya pamoja.
Wafanyakazi
 wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu duniani 
(UNFPA) hapa nchini,  wadau wa Tushikamane Pamoja Foundation pamoja 
madaktari vijana wanaounda kundi la Projeckt Inspire chini ya mradi wa 
Inspire Healthy kwenye picha ya pamoja na mmoja wa wazee wanaoishi 
kituoni hapo.










No comments:
Post a Comment