Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Monday, November 1, 2010

..

Huduma ya Vodafone M-PESA yaongoza kimataifa

Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania imetajwa kuwa ni kampuni bora kwa utumaji wa fedha ulimwenguni kupitia huduma yake ya Vodafone M-Pesa.
Taarifa hiyo ilitolewa ilitolewa wakati wa maonyesho ya kwanza yanaohusu huduma za utumaji pesa kwa njia ya simu za mkononi yaliyofanyika Dubai tarehe 25 mwezi huu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Dietlof Mare alisema taarifa hiyo iliyopatikana wakati wa maonyesho hayo imeipa faraja kampuni yake .
“Taarifa hiyo inatambua mchango na viwango vya huduma zetu kwa wateja pia , alisema Mkurugenzi hiyo
Bw. Mare alisema kwamba Kampuni hiyo haitabweteka kwa sababu imepata heshima hiyo kubwa Ulimwenguni kwa wa watoaji kwa huduma na bidhaa bora na badala yake itaboresha huduma zake.
Hivi karibuni kampuni hiyo ilishinda tunzo ya Chapa Bora kwa Afrika Mashariki , ili kushinda tunzo hiyo vigezo mbalimbali huzingatiwa ikiwamo unora wa bidhaa.
Bw. Mare aliwashukuru wateja wote wa Vodacom kwa uaminifu wao na kuwahakikishia kwamba wataendelea kuwapatia huduma bora wateja wake ili waweze kukata kiu yao ya mawasiliano na sanjari na huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo.
“Tutaendelea kuwapatia wateja wetu huduma bora ambazo zitakidhi kiu yao ya mwasiliano lakini katika hali ambayo wataimudu na yenye manufaa kwao,”
Vodafone M-PESA, ni njia rahisi ya utumaji pesa kwa njia ya simu za mkononi, njia hi ilizinduliwa rasmi mwaka 2008, kwa hapa nchini huduma hiyo imekubalika na inatumiwa na Watanzania wengi.
Wateja wa Vodafone-MPESA sasa wanaweza kulipia huduma mbalimbali kama vile LUKU, bili za Dawasco, kuongeza muda wa maongezi, kutuma na kupokea fedha kwenda mtandao wowote hapa nchini na kulipa ada za wanafunzi.
Hadi sasa huduma hiyo ina wateja zaidi ya milioni 5.4 waliojisajili sajiliwa katika huduma, huku kila mwezi wateja wapya 500,000 wakisajiliwa.
Hivi sasa zaidi ya shilingi bilioni mia sita 600 zimeshatumwa kupitia mtandao huo huku idadi ya mawa

No comments: