Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Friday, November 5, 2010

WABUNIFU KADHAA WASHUKA DAR KWAAJILI YA SWAHILI FASHION WEEK

Baadhi ya Wabunifu wa Mavazi watakaoshiriki katika Swahili Fashion Week wakiwa katika picha ya pamoja.

Jukwaa la tatu la Swahili fashion Week linaanza leo katika viwanja vya karimjee jijini Dar es salaam na kudumu kwa muda wa siku tatu hadi tarehe 6 ya mwezi wa November 2010.
Katika jukwaa la mwaka huu jumla ya wabunifu 24 kutoka nchi za Afrika hasa zile zinazozungumza lugha ya Kiswahili wamejiandaa vya kutosha katika kuonesha kazi zenye viwango vya kimataifa.
“Tunashukuru kwani mipango yote inakwend kama tulivyopanga na tayari wabunifu wote wamefika kwa ajili ya shoo kabambe ambapo itakuwa na tofauti kubwa kulinganisha na zile zilizopita. Tayari wabunifu wote 24 kutoka Tanzania na nchi za Pan Afrika wapo tayari kwa shoo ya mwaka, inayoandaliwa nyumbani mwa Swahili Fashion Week.” Alisema Mustafa Hassanali muandaaji wa Swahili Fashion Week
“Kwa mara nyingine tena tupo na Swahili Fashion Week 2010, na kusaidia kukuza Sanaa ya ubunifu wa mavazi hapa nchini, pamoja na kuwakaribisha wageni wetu ambao ni wabunifu wa kimataifa. Southern Sun inajivunia kutokana na mchango wake inayotoa kwa Sanaa ya ubunifu wa mavazi Afrika na hii intupa fursa ya kuendelea kwa njia mbalimbali.” Alisema meneja mkuu wa southern sun Hotel Ndugu Adam fuller
Southern Sun hotel imekuwa nyumba ya Swahili Fashion Week toka mwaka 2009.
Swahili Fashion Week inafanyika kwa mwaka watatu sasa na itawashirikisha wabunifu 24 ambapo kwa mujibu wa ratiba, siku ya kwanza shoo itapambwa na Manju Msita (Tanzania),Sonu Sharma (Kenya),Shelina Ebrahim (Tanzania/Canada),United Against Malaria (Tanzania Various),Farha Sultan (Tanzania),Tanzania Mitindo House (Tanzania - Various), KemiKalikawe (Tanzania) na Asia Idarous (Tanzania)
Kwa upande wa tarehe tano, siku ya ijumaa mwanamitindo kutoka Tanzania Jamila Vera Swai tfungua pazia akifuatiwa na Marinella Rodriguez (Mozambique),Stella Atal (Uganda),Kooroo (Kenya),Zamda George (Tanzania),Mafi Designs (Ethiopia),Moo Cow (Kenya),Robi Morro (Tanzania),Made by Africa (Tanzania) na Asos Africa (UK)
Tarehe sita November siku ya mwisho ya jukwaa la Swahili Fashion Week, wabunifu wtakoonesha kazi zao ni pamoj na wabunifu wanane wanaochipukia waliofanikiwa kuingia fainali kupitia shindano la wabunifu wanaochipukia, Emerging Designers Competition (Tanzania - Various),Gabriel Mollel (Tanzania),Khadija Mwanamboka (Tanzania),KikoRomeo (Kenya), John Kaveke (Kenya), Chichia London (Tanzania/UK), Ailinda Sawe (Tanzania)
“ Pamoja na kuwakaribisha wageni wetu ambao ni wabinifu wa mavazi , pia Southern itatoa zawadi kwa gauni bora katika Swahili Fashion Week kwa huu , lengo ni kusaidia kukuza Sanaa ya ubunifu wa mavazi” Aliongeza Saphia Ngalapi, Swahili Fashion Week PR manager

No comments: