Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Friday, March 4, 2011

MODEL OF A WEEK !!

Shauna kaye-jamaican sexy model


UZINDUZI WA EXTRA BONGO
Wanenguaji wa bendi YA EXTRA BONGO wakipiga picha ya pamoja ukumbini humo. Na hii ndiyo safu kamili ya wanenguaji wa bendi hiyo inayoongozwa na Ally Choki 'Mzee wa Farasi'.


Toure anatumia "dawa za kuongeza nguvu"

Beki wa Manchester Kolo Toure amesitishwa kucheza soka baada ya kupimwa na kugundua alitumia dawa inayotambuliwa, specified substance.
Kolo Toure
Kolo Toure
Mchezaji huyo, mwenye umri wa miaka 29, aliarifiwa na chama cha soka cha England, FA, kwamba iligunduliwa alitumia dawa hiyo mwezi uliopita, wakati timu yake ilipocheza dhidi ya Manchester United, na yeye akiwa ni mchezaji wa zamu, licha ya kutopewa nafasi kucheza katika mechi hiyo.
Shirika la kupambana na dawa zilizopigwa marufuku World Anti-Doping Agency, WADA,' lilisema dawa hiyo ni mojawapo ya dawa zinazoweza kutumiwa kama dawa ya kawaida tu na basi sio mojawapo ya zile zilizopigwa marufuku.
Adhabu inayoweza kutolewa na shirika la kimataifa la kuzuia utumizi wa madawa ya kuongezea nguvu michezoni, WADA, haijulikani.
Huenda likatoa onyo, ama kumuadhibu kwa kumpiga marufuku asicheze kwa kipindi cha hata miaka miwili.
Kolo Toure upande wa kulia
Kolo Toure upande wa kulia
Shirika hilo limeelezea kwamba limemsimamisha asicheze baada ya kugundua alitumia specified substance, likimaanisha kwamba licha ya ushahidi kupatikana kwamba alitumia dawa hiyo, huenda ikawa sio kupitia njia ya moja kwa moja ya kuitumia kama dawa ya kuongezea nguvu michezoni, lakini huenda ikawa mwilini kupitia njia nyinginezo.
Klabu ya Manchester City imethibitisha kwmaba Toure amesitishwa kucheza soka, huku wakisubiri utaratibu wa kisheria utakwenda vipi.
Toure ana hadi tarehe 9 Machi kuamua iwapo anataka sampuli ya pili ipimwe.
Lakini, iwapo hatapimwa tena basi itabidi akabidhi maelezo na atakabiliwa na taratibu ya adhabu itakayochukua muda mrefu.

SHILOLE ATANGAZA VITA NA WALA VIRINGI

 
Msanii chipukizi wa filamu Zena mohamed "shilole" amethubutu kudai kwa kukieleza moja vyombo vya habari kuwa hashobokei mapapaa"wala viringi".
Licha ya binti huyo kuwa na shepu ya kuwastua wanaume wengi wenye fedha zao hapa mjini shilole kadai sio limbukeni wa kushobokea mafweza ana true love kwa muhusika wake.
Hebu tufuatilie kwa kina kama miezi kadhaa atadumisha hiyo kauli yake kwani kujigamba huko kumewakwaza sana wakwale hao.

No comments: