Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, March 23, 2011

WYCLEF JEAN ALIDANGANYA KUPIGWA RISASI


Polisi nchini Haiti wamefunguka kuwa madai ya Rapper na Mwanaharakati, Wyclef Jean aliyedai kuwa amepigwa risasi mkononi siku ya mkesha wa Uchamkuzi mkuu nchini humo,si ya kweli.

Mkuu wa Jeshi la Polisi la Haiti,Vanel Lacroix amesema kuwa Wyclef alipata majeraha baada ya kudondokewa na vipande vya kioo lakini anashangaa imekuaje amesema kuwa amepata jeraha la risasi.
Mkuu huyo alifunguka zaidi na kusema “tulikutana na daktari aliyemtibu na kutuambia kuwa alikatwa na vioo na sio jeraha la risasi” na kusema story hii ni yakutengeneza tu wala “sio kweli”

Inaelekea mwana alitengeneza story ili aweke attention kwa mshikaji wake,Michael Martelly ambaye pia ni mwanamuziki,aliyegombea Urais wa Haiti baada ya Wyclef kuwekewa kipingamizi na inasemekana kuwa alisaidia kifedha.

Moshi mwengine wazuka kwenye vinu vya nyuklia

Huku wahandisi wa Kijapani wakijitihidi kuvirekebisha vinu vya nyuklia ili kudhibiti kupenya kwa mionzi yenye sumu huko Fukushima, serikali imelazimika kuwaondoa wafanyakazi wake katika eneo hilo kwa kuhofia usalama wao.


Shirika la Habari la Ujerumani (DPA) limeripoti kuonekana kwa moshi mzito leo hii (Jumatano, 23.03.2011), ukitoka kwenye jengo la kinu namba 3, na kusababisha wafanyakazi wa kinu hicho, wale waliokuwa kwenye kinu chengine namba 4 pamoja na wafanyakazi wa huduma za uokozi kuhamishwa kwa usalama wao.
Kamisheni ya usalama wa nyuklia ya Japan imesema  hadi sasa chanzo cha moshi huo hakijajuilikana.
Kwa mujibu Shirika la Habari la Reuters, kiwango cha mionzi katika kinu hicho kilikuwa kimepanda hadi kipimo cha 435 masaa mawili kabla ya moshi kuonekana, lakini kikashuka hadi 283 baada ya moshi kuanza kufuka.
Hata hivyo, vipimo vyote viwili ni vikubwa sana, ikilinganishwa na hali ilivyokuwa kwa siku chache zilizopita.
Mbogamboga kutoka Kaginawa, JapanBildunterschrift: Großansicht des Bildes mit der Bildunterschrift:  Mbogamboga kutoka Kaginawa, JapanHapo jana, mafundi wa Shirika la Umeme la Japan walifanikiwa kuunganisha umeme kutoka nje ya vinu vyote sita, jambo ambalo lingeliweza kuwasaidia wahandisi kuufanyia marekebisho mfumo wa kupozea mashine wa kinu namba 3.
Mionzi kwenye maji
Nako katika mji mkuu wa Tokyo, kiwango cha mionzi kinachozidi vipimo vinavyochukuliwa kuwa salama kwa watoto, kimegundulika kwenye maji ya mifereji, na kusababisha maafisa wa mji huo kuwashauri wazazi kutokuwaruhusu watoto wao kunywa maji hayo.


MIILI YA WASNII WALIOPATA AJARI WA 5 STARS
Hawa ni marehemu waliokufa kwenye ajali hiyo na mwili wa tatu ndio Issa Kijoti aliyekuwa mwimbaji mzuri kabisa katika bendi hiyo ya Five Star Mordem Taarabu

Picha hizi ni kwa hisani ya Salim Chuma



Adebayor kuichezea tena Togo

Soka ya Togo imepokea habari muhimu za kupendeza kwamba kocha Stephen Keshi na mshambuliaji Emmanuel Adebayor wameamua kurejea katika timu ya taifa.
Emanuel Adebayor
Emanuel Adebayor
Adebayor anayechezea Real Madrid, aliamua kuacha kuchezea timu ya taifa baada ya shambulio la risasi lililoelekezwa katika basi la wachezaji wa Togo, wakati wa mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Angola 2010, ambao watu wawili waliuawa.
Adebayor tayari amelihakikishia Shirikisho la Soka la Togo, atacheza siku ya Jumamosi dhidi ya Malawi katika kundi lao la K.
Kocha Keshi raia wa Nigeria tayari yupo nchini Togo akichukua nafasi ya kocha Mfaransa Thierry Froger.
Keshi alizozana na Shirikisho la Soka la Togo mwaka 2006 baada ya mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, kabla ya kuanza kwa fainali za Kombe la Dunia mwaka 2006.
Lakini Keshi, ambaye bado hajasaini mkataba na Shirikisho la Soka la Togo, anarudi kwa mara ya tatu baada ya Froger kujiuzulu kwa vile amepata kazi ya kuifundisha timu ya Nimes ya Ufaransa mapema mwezi huu.
Adebayor pia alijiondoa kuichezea timu ya taifa ya Togo, miezi mitatu baada ya waasi wa jimbo la Cabinda kushambulia kaskazini mwa Angola na kuleta kizaazaa ambapo timu hiyo ilijitoa katika mashindano ya Mataifa ya Afrika 2010.
"Nimepima tena mawazo yangu kwa muda wa miezi sasa tangu shambulio la Angola," Alisema mwezi wa Aprili mwaka 2010.
"Ni tukio ambalo siwezi kulisahau na nisingependa kukutana nalo tena."
Lakini baada ya kusafiri hadi Madrid kukutana na Adebayor, Rais wa Shirikisho la Soka la Togo, Gabriel Ameyi amesema amepokea habari nzuri kutoka kwa nahodha huyo wa zamani wa Togo na sasa ameamua kumaliza kuisusia timu ya taifa.
Adebayor atasafiri moja kwa moja hadi Malawi akitokea Ulaya kwa ajili ya mechi hiyo.

Chris Brown Arrested Over GMA?!

0322_chris_brown_EX

Where are Chris Brown's handlers? The boy reportedly dumbed out on Good Morning America just this morning after they asked him about Rihanna. You would think his people would have media trained him for this stuff. According to TMZ, Brown dumbed out after the interview, not during. He went into his dressing room screaming and broke a window. Security was eventually called and when they got there, he had torn his shirt off. He was supposed to do a performance for another ABC-owned entity, but he bounced. eportedly exploded in rage behind the scenes at ‘Good Morning America’ this morning. This could be an exaggeration, but they said on the way out, Chris got in the face of a producer like he was going to do something, but he left.

UPDATE: It looks like Chris Brown has been arrested for the outburst. Remember dude is on probation over the whole Rihanna thing...so this is a problem.

UPDATE #2: It has been reported that CB knew that he would be asked about Rihanna. This new has lead to speculation that this is a mere play for press.





Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii jana ilikutana jijini Dar es Salaam na Uongozi wa Wizara ya Habari ,Vijana, Utamaduni na Michezo kwa dhumuni la kufahamiana na kubadilishana mawazo kiutendaji kabla ya kuanza kazi rasmi . Kamati hiyo ikiongozwa na Mwenyekiti wake Jenista Mhagana pamoja na Makamu wake Juma Nkamia.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo Sethi Kamuhanda akitoa taarifa ya Wizara yake Machi 22,2011 mbele ya Kamati ya Maendeleo ya Jamii jijini Dar ea Salaam ilipokutana na kwaajili ya kufahamiana na kubadilishana mawazo kiutendaji kabla ya kuanza kazi rasmi.
Mbunge wa Mbeya mjini Mh. Joseph Mbilinyi akichangia mada katika mkutano huo.
Mmoja wa wajumbe katika mkutano huo Bw. Helman Hokororo kutoka Idara ya Habari Maelezo akichangia hoja katika mkutano huo.Picha na Mwanakombo Jumaa - MAELEZO

Vikwazo vya kwenda kusoma Uingereza


Maandamano ya wanafunzi Uingereza
Sheria za kupata viza za wanafunzi nchini Uingereza zinatarajiwa kuwa ngumu zaidi- baada ya kuibuka wasiwasi kuwa mbinu za kuingia nchini humo kwa minajil hiyo hutumiwa kiudanganyifu
Waziri wa mambo ya ndani Theresa May alisema viza za wanafunzi hazitumiwi inavyotakiwa na "wengi wamekuja hapa kufanya kazi na si kusoma".
Alitangaza mpango wa kupunguza idadi ya viza za wanafunzi kufikia 80,000- takriban robo ya idadi iliyopo sasa.
Waziri kivuli wa wizara ya mambo ya ndani Yvette Cooper alionya sheria hazitakiwi kuharibu idara zenye thamani ya dola za kimarekani bilioni tano kwa mwaka.
Bi May aliliambia bunge kuwa matumizi mabaya ya viza za wanafunzi yamekuwa "ishara ya mfumo wa uhamiaji uliotumiwa vibaya".

Sheria za lugha

Sheria ngumu zilizowekwa ni pamoja na mwanafunzi kutakiwa kuzungumza lugha ya Kiingereza.
Bi May alisema alitaka kumaliza tatizo ambapo wale wanaojifanya wanafunzi hufika kwenye uwanja wa ndege wa Uingereza na kushindwa hata kutaja masomo wanayotarajia kufanya.
Pia utaratibu utazidi kubanwa kwenye kuwaruhusu wanaolelewa na mwanafunzi huyo kujiunga naye Uingereza- na idadi ya miaka ya wanafunzi kutoka nje kukaa Uingereza baada ya kumaliza masomo yao itapunguzwa.
Katika kukabiliana na wasiwasi wa viza za wanafunzi kutumiwa vibaya na wahamiaji wa kiuchumi, kutakuwa na kiwango maalum cha saa za kufanya kazi kwa wanafunzi kutoka nje.
Awali vyuo vikuu vilionyesha wasiwasi wa kupoteza wanafunzi kutoka nchi za nje kutokana na sheria kali za kuomba viza.
Vikwazo vingi vinawalenga wanafunzi walio katika vyuo vya watu binafsi badala ya vyuo vikuu.
Hata hivyo Bi May aliwaambia wabunge kwamba "njia kama hiyo" ya kusoma kupitia vyuo vikuu vitalindwa, iwapo tu vyuo vikuu vitawadhamini wanafunzi.

STYLE MOTO MOTO MARCH IMEPAMBA MOTOOOO

MBUNIFU GABRIEL MOLLEL KAZINI NA WANAMITINDO OM JOSH, ALEXIA NA MISS TANZANIA


WANAMITINDO NA MBUNIFU MPYA ESKADO BIRD AKIBADILISHANA NAMBA NA JAMIRA NYANGASA


MBUNIFU ATAKAE BEBA STYLE MOTO MOTO MARCH 25 GABRIEL MOLLEL KATIKA POZI NA JAMILA NYANGASA


WANAMITINDO WAKIONDOKA MA MBUNIFU MARTIN KADINDA

STYLE MOTO MOTO INADHAMINIWA NA VODACOM TANZANIA,REDD'S,QUICK PRINT,VAYLE SPRINGS,EVENT LITES,UNIQUE PEARL COLLECTION,MIMI'S COLLECTION AMINA DESIGN NA HOTELI YA DOUBLE TREE

Majeshi washirika yaungana Libya


Gari la waasi Libya
Watu walioshuhudiwa walisema, majeshi ya kimataifa yameanza mashambulio mapya ya anga karibu na mji uliopo magharibi mwa Libya wa Misrata unaoshikiliwa na waasi.
Awali majeshi yanayomtii Kanali Gaddafi yaliondoka eneo hilo, lakini wakazi wa Misrata walisema wadunguaji wameendelea kuwalenga watu wakiwa juu ya majengo.
Kulingana na taarifa zilizotolewa majeshi ya Kanali Gaddafi pia yalianza kuchakaza mji wa Zintan, karibu na mpaka wa Tunisia.
Mapigano hayo yameanza huku nchi za magharibi zikijadiliana ya nani anaongoza harakati za kuingilia kati mzozo wa Libya, huku Marekani ikipendelea zaidi kukabidhi jukumu hilo kwa majeshi ya umoja wa nchi za kujihami za Ulaya, Nato.
Mkazi mmoja wa Misrata aliiambia Reuters kwa simu: "Asubuhi hii, mashambulio mawili ya ndege yamefanyika kwenye kituo cha kikosi maalum cha Gaddafi.
"Watu wawili waliuawa na wadunguaji saa moja iliyopita katikati ya mji. Miili yao sasa iko hospitali, nimewatembelea muda si mrefu. Ufyatulianaji risasi bado unaendelea."
Daktari mmoja kwenye mji huo alisema kuwa wandunguaji walikuwa wakiendelea kuwapiga risasi raia, na kuthibitisha kuwa takriban mtu mmoja alikufa.

MODEL OF A WEK-Nina Mascunana : Spanish – Chinese – Filipina Model

Mini Biography of Nina Mascunana
Birth Date: 11-11-1986
Hometown: LA
Ethnicity: Spanish-Chinese-Filipino
Height:5′1
Weight: 98
Measurements: 34C-24-36
Hair: Long dark brown
Eyes: brown
Photographer Credits:
Mike Brochu, Exotic Flights, Kenneth Braydon, Lowrider Magazine, Norm Fischer, Harvey Butts, Performance Auto & Sound, Orlando Perez, Open Your Eyes
Nina Mascunana is by far one of the most beautiful models that I have seen. It definitely has something to do with her exotic roots, being that she is Spanish Chinese and Filipino.
Despite her beauty, Nina is a very simple person who thrives to achieve her life long goals.Not only is she amazingly beautiful, she’s also intelligent.
Nina recently graduated from nursing school and has set out to become a registered nurse.
Nina enjoys spending her free time with family and friends. Some of Nina’s hobbies include exercising, dancing, and most of all, eating!

POZI LA WIKI HII KATIKA PICHA
Mexican model
hizi ni swagga sio nyasi mtu mzima.  click older post upate previouz kibao tu

No comments: