Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, February 9, 2011

 

Mechi za Ubingwa wa Afrika zaahirishwa

Mechi kadha za Ubingwa wa vilabu barani Afrika zimeaahirishwa kutokana na kuendelea kwa mashindano ya Chan .

Shirikisho la Soka barani Afrika, Caf, imeahirisha mechi kadha za kutafuta klabu bingwa zilizopangwa kuchezwa mwishoni mwa wiki hii.
Mechi zitakazoathirika ni za vilabu vyenye wachezaji takriban watatu wanaoshiriki mashindano ya kutafuta bingwa wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani, yanayoendelea nchini Sudan.
Katika mechi zote tisa za Ubingwa wa vilabu, sasa zitachezwa katika tarehe itakayopangwa baadae, wakati mechi nyingine sita za kuwania Kombe la Shirikisho pia nazo zimeathiriwa na mashindano ya Chan.
Taarifa iliyotolewa na Caf imesema mechi hizo sasa zitachezwa wiki ya mwisho ya mwezi wa Februari.
Mechi zifuatazo zimeahirishwa:
Ubingwa wa Vilabu Afrika
JC Abidjan (CIV) v ASFAN (NIG)
Astres Douala (CMR) v US Bitam (GAB)
Djoliba (MLI) v East End Lions (SLE)
Cansado (MTN) v ASEC Mimosas (CIV)
Club Africain (TUN) v. APR (RWA)
Aduana Stars (GHA) v Wydad Casablanca (MAR)
Cotonsport Garoua (CMR) v Vital'O (BDI)
Vita Club (COD) v Ocean View (ZAN)
Zamalek (EGY) v Ulinzi Stars (KEN)
Kombe la Shirikisho Afrika:
AS Real (MLI) v Tevragh Zeina (MTN)
Sahel (NIG) v Dynamic (TOG)
AshantiGold (GHA) v Sewe San Pedro (CIV)
Africa Sport (CIV) v Sequence (GUI)
Inter Stars (BDI) v Missile (GAB)
DC Motema Pembe (COD) v KMKM (ZAN)



Justin Bieber Is a Gentleman, Buys Selena Gomez an Ice Cream Cone

ustin Bieber and Selena Gomez were spotted holding hands at Santa Monica Pier on Sunday, and they reportedly stopped for ice cream while on their romantic stroll. Justin was the perfect gentleman and insisted on paying for the 18-year-old Disney star's tasty treat.

An onlooker revealed: "Selena ordered a kid's chocolate ice cream in a sugar cone. She tried to pay with her credit card, but Justin took it out of her hand and gave his card instead.

"Justin didn't order anything. They were really quiet. Honestly, they seemed like very ordinary people."

Despite the low-key setting for their first public date, 16-year-old Justin and Selena reportedly attracted quite a crowd of fans eager to learn whether they were a fully-fledged couple.

The source added to HollywoodLife.com: "They were quite the spectacle. Everyone was whispering and snapping pics and videos with their phones."

With the pair having been spotted on a string of dates in recent weeks, Justin admitted Selena was one of his "best friends."

When asked what he should say to people who have seen the pair in an intimate setting, the singer replied: "Just tell them that she's, like, one of my best friends."

See more Justin Bieber and Selena Gomez pics here:
Justin+Bieber in Justin Bieber and Selena Gomez at the Santa 
Monica Pier

 

 MASHINDANO YA NYAMA CHOMA YAZINDURIWA


Meneja wa Bia ya Safari Lager,Fimbo Buttallah (kati) akifafanua jambi wa wakti wa uzinduzi wa mashindano ya kuchoma nyama yajulikanayo kama "Safari Lager Nyama Choma"katika pub iliyopo ndani ya kampuni ya bia Tanzania,jijini Dar.kulia na kushoto ni majaji wa mashindano hayo.

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager leo imezindua rasmi yale mashindano ya aina yake na ya kuvutia ya kuchoma nyama yajulikanayo kama “Safari Lager Nyama Choma”

Mashindano haya hushirikisha majiko ya baa mbalimbali katika umahiri wa kuchoma nyama na hatimaye zawadi hutolewa kwa washindi.

Akizungumza katika uzinduzi wa mashindano ya mwaka huu, meneja wa Bia ya Safari Lager Bw. Fimbo Butallah alisema; madhumuni makubwa kwa bia ya Safari lager kuendesha mashindano haya ambayo yamekuwa kivutio kwa walaji wa nyama na watumiaji wa bia ni kuhakikisha tunaleta changamoto kwa majiko yanayochoma nyama, ili kuhakikisha walaji wanapata kile kilicho bora kabisa. Watumiaji wa bia ya Safari Lager, hupendelea sana kuitumia huku wakisindikiza na nyama choma iliyoandaliwa vizuri, hivyo kupitia mashindano haya, bia ya Safari Lager inaendeleza utamaduni wa kunywa bia na kula nyama. Kufuatia ubora wa hali ya juu wa bia ya Safari lager, tunafurahi sana pale ambapo mywaji atapata pia nyama iliyo bora ili mtumiaji aweze kuridhika zaidi.


Sudan kuwa taifa huru na jipya


Maafisa wa uchaguzi wamethibitisha matokeo ya kura ya Sudan Kusini kujipatia uhuru.
Matokeo
Kusini wachagua kujitawala
Maafisa hao wamesema karibu asilimia 99 ya wapiga kura wametaka nchi hiyo kujitenga na upande wa Kaskazini.
Kura hiyo ni sehemu ya makubaliano ya amani ya mwaka 2005, yaliyomaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa miongo miwili.
Ingawa upigaji kura ulifanyika kwa amani, hali ya wasiwasi bado ipo katika maeneo yenye utajiri wa mafuta.
Watu wasiopungua 50 waliuawa mwishoni mwa wiki, katika mapigano baina ya wanajeshi wa jimbo la Upper Nile la Sudan Kusini.

Kujitawala

Mapigano hayo yalitokea kati ya wanajeshi wa Kaskazini, kuhusiana na mzozo wa nani abakie na silaha nzito nzito, wakati vifaa vikihamishwa kuelekea kaskazini katika mpaka mpya.
Kura
Karatasi za kura Sudan Kusini
Maafisa wa uchaguzi wamesema asilimia 98.83 ya wapiga kura wa Sudan Kusini wameunga mkono nchi hiyo kujitawala.
Kabla ya tangazo hilo la matokeo mjini Khartoum, rais Omar al-Bashir alisisitiza tena kuwa atakubaliana na matokeo ya kura hiyo.
Bashir
Omar al-Bashir
"Tunakubali na kuyapokea matokeo hayo kwa sababu yanawasilisha matakwa ya watu wa Sudan Kusini," amesema rais Bashir kupitia televisheni ya taifa.
Mwandishi wa BBC mjini Khartoum anasema Bw Bashir aliwahi kutoa matamshi kama hayo siku za nyuma, lakini tamko hili la kusisitiza litawahakikishia watu wa Kusini walio na mashaka ya kuwa huenda upande wa Kaskazini ukabadili msimamo wake.
Rais huyo amesema ana nia ya kuwa na uhusiano mwema na taifa lijalo la Kusini. Marekani imesema itaiondoa Sudan katika orodha ya nchi inayozituhumu kwa kusaidia ugaidi, iwapo kura hiyo itakwenda salama.
Matokeo
wananchi wakishangilia matokeo
Mwandishi wa BBC Nyambura Wambugu akiwa Torit anasema baada ya tangazo kutolewa, wananchi wa huko wametoka nje na kuanza kusherekea kwa kucheza muziki.
"Sasa mimi ni raia wa daraja la kwanza katika nchi yangu" amesema Abiong Nyok, mama wa nyumbani akizungumza na BBC.

Kubaguliwa

Nusu karne iliyopita, raia wa kusini wamepigana vita mara mbili vya wenyewe kwa wenyewe na upande wa kaskazini, ambapo watu zaidi ya milioni mbili wanakadiriwa kufa.
Upande wa Kusini inajiona kama una tofauti za kitamaduni, kidini na kikabila na upande wa Kaskazini, na kusini inaamini imepitia miaka mingi ya kubaguliwa.
Taarifa zinasema kutangazwa na matokeo haya ya mwisho sio mwisho wa mchakato wote.

Changamoto

Masuala yakiwemo eneo la mpakani la Abiyei, uraia, masuala ya kisheria na rasilimali kama vile mafuta, yatahitaji kujadiliwa.
Ingawa ni tajiri kwa mafuta, Sudan Kusini ni moja ya maeneo yenye maendeleo duni zaidi duniani, na mvutano wa kikabila na uhusiano tete na upande wa kaskazini vitaleta changamoto za kiusalama kwa kipindi kirefu.

No comments: