Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Sunday, November 13, 2011

TFF YAWAPA ONYO LA MWISHO RAGE NA SENDEU



  Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imetoa onyo la mwisho kwa Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage na Ofisa Habari wa Yanga Louis Sendeu kutokana na kutohudhuria vikao viwili mfululizo kama walivyotakiwa na kamati hiyo.

 Rage na Sendeu wanatakiwa kujieleza mbele ya kamati hiyo iliyo chini ya Kamishna mstaafu wa Polisi, (CP), Alfred Tibaigana, kutokana na tuhuma za utovu wa nidhamu baada ya kudaiwa kutoa kauli zenye lengo la kushusha maendeleo ya soka hapa nchini, wakati wa kuelekea mechi ya Ngao ya Hisani, kati ya Simba na Yanga.

  Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, kamati hiyo inatarajiwa kukaa hivi karibuni ambapo imeagiza Rage ataarifiwe kuwa anayepanga vikao vya kamati hiyo sio yeye, hivyo endapo hatatokea siku atakayoitwa, atajadiliwa na mamuzi kutolewa.

 AMASHA LA STR8 MUSIC INTER COLLEGE 2011-DODOMA
Msanii Barnaba akifanya show katika tamsha la STR8 MUZIK INTER COLLEGE SPECIAL 2011 katika Viwanja vya Royal Village
Walimbwende wakiserebuka ngoma za Juma Nature aka Kibra wakati alipopanda jukwaani
Mashabiki wakiwa wamefurika kwenye viwanja vya Royal Village mjini Dodoma usiku wa kuamkia leo

NAIBU WAZIRI VIWANDA NA BIASHARA AFUNGUA RASMI MAONESHO YA SIDO YA NYANDA ZA JUU KUSINI MKOANI RUKWA

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Lazaro Nyarandu (MB) akikata utepe kama ishara ya kufungua rasmi maonyesho ya 9 ya SIDO ya nyanda za juu kusini inayoshirikisha mikoa ya Rukwa, Iringa na Mbeya. Kulia kwake anayeshuhudia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Joyce Mgana. Maonyesho hayo yanafanyika katika Uwanja wa Nelson Mandela Mkoani Rukwa kwa kushirikisha wajasiriamali kutoka zaidi ya mikoa 14 nchini na wengine kutoka nchi jirani za Kenya na Burundi.
Mkurugenzi Mkuu wa SIDO nchini Ndugu Mike Laizer akifafanua jambo kwa Naibu wa Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Lazaro Nyarandu kwenye banda la SIDO. Kulia kwa Naibu Waziri ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Joyce Mgana.

Uhifadhi wa Mazingira nao umepewa kipaumbele Mkoani Rukwa, Mjasiriamali wa uhifadhi wa Mazingira wa kikundi cha REYO akinadi miti aina mbalimbali inayofaa kwa uhifadhi wa mazingira na matumizi mengineyo katika maonesho hayo.
Maonyesho hayo yakiendelea

Mjasiriamali wa Rukwa anayejishughulisha na utengenezaji wa viatu kwa kutumia ngozi mbalimbali. Chipawas Leather Tunning wanapatikana maeneo ya Jangwani Wilayani Sumbawanga, wapo pia kwenye maonesho hayo. 

No comments: