Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, February 1, 2012

HUDUMA ZA KLINIKI ZASITISHWA MUHIMBILI

MGOMO wa madaktari umezidi kutikisa na kuathiri huduma za afya katika hospitali kuu nchini, huku Taasisi ya Mifupa (Moi) ikitangaza rasmi kufunga kliniki zote zinazohudumia wagonjwa wa nje hadi mgomo huo utakapomalizika.Mkurugenzi Mtendaji wa Moi, Profesa Lawrence Museru alitangaza uamuzi huo wa kufunga huduma hizo jana, akisema taasisi hiyo ina madaktari bingwa 30 pekee na ndiyo wanaofanya kazi huku madaktari wake wengine zaidi ya 30 wakiwa kwenye mgomo. Alisema kufuatia hatua hiyo, madaktari waliobaki hawawezi kujigawa na kuhudumia wagonjwa wote wanaofika katika taasisi hiyo na ndiyo sababu, wamelazimika kusitisha huduma kwa kliniki.

No comments: