Mwananchi huyu mwenye hasira kali akimnyanyua juu kibaka huyo na kumtupa chini kama akina 'John Cena'.
..Kichapo kikiendelea kwa kibaka huyo.
Kibaka huyo akizidi kuhukumiwa mtaani.
Ustadhi akijaribu kumnusuru kibaka huyo.
Ustadhi huyo aliamua kuondoka na kibaka ili kumwokoa.
Akimpeleka kituo kikuu cha polisi kilichopo jirani na eneo hilo la Shani.
KIJANA mmoja anayesadikiwa kuwa ni kibaka mchana huu amenusurika kifo 
baada ya kupokea kichapo kikali kutoka kwa wananachi wenye hasira 
wakimshutumu kuiba watoto wadogo na kwenda nao eneo la mto Morogoro  
chini ya daraja la Shani na kuwafanyia vitendo vya kihuni.
Akizungumza na Mtandao huu mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa 
jina la Juma Athuman alidai kwamba kijana huyo ana kawaida ya kuwateka 
watoto wadogo hasa wa shule na kuwapeleka chini ya daraja hilo na 
kuwafanyia vitendo vya kihuni.
" Kwa kipindi kirefu tulikuwa tukimsaka kibaka huyu ambaye ana tabia ya 
kuwateka watoto wadogo na kuwapeleka mto wa Morogoro chini ya daraja la 
Shani.
"Muda huu tumemfuma akiwa chini ya daraja hilo na mtoto mdogo ndipo 
tulipomfukuza na kufanikiwa kumkamata eneo hili la kituo cha mafuta 
jirani na daraja hili la Shani," alisema Juma Athuman.
 
 
No comments:
Post a Comment