WAKATI kukiwa na tetesi kuwa lile kundi la muziki wa bongo fleva Pah One, limevunjika
 meneja wa kundi hilo amekana ishu hiyo na kudai kuwa kundi bado 
lipo lakini kikubwa ambacho kilitokea ni kutokuelewana ndipo baadhi ya 
wasanii walipoamua kusafiri na kubaki wawili na watakaporejea 
wataendelea kama kawaida.
Kundi hilo linaundwa na vijana wanne ambao ni Nahreel , Ola, Aika na Igwee ambao wamekuwa wakifanya muziki wa tofauti ambao unaweza kuwatambulisha zaidi hata kimataifa.
Hata hivyo meneja huyo alipotakiwa kujitambulisha jina lake alidai huwa hapendi jina lake litokee kwenye vyombo vya habari na kitu anachokifanya yenye ni kuwasaidia vijana.
Kundi hilo linaundwa na vijana wanne ambao ni Nahreel , Ola, Aika na Igwee ambao wamekuwa wakifanya muziki wa tofauti ambao unaweza kuwatambulisha zaidi hata kimataifa.
Hata hivyo meneja huyo alipotakiwa kujitambulisha jina lake alidai huwa hapendi jina lake litokee kwenye vyombo vya habari na kitu anachokifanya yenye ni kuwasaidia vijana.
 
 

No comments:
Post a Comment