
KUNDI
 la wananchi wanaodaiwa kuwa na hasira, wamevamia kituo cha Polisi cha 
Kibiti Wilayani Rufiji na kufanya vurugu kubwa baada ya raia mmoja kufa 
kwa kile kilichodaiwa kipigo cha Polisi.
Chanzo
 chetu cha Habari kutoka Kibiti kinaipasha kuwa kijana aliyefariki 
kutokana na kipigo hicho ni Hamis Mpondi, ambaye mauti yamemfika wakati 
akipatiwa matibabu Hospitali ya Muhimbili.
Habari
 zaidi zinapasha kuwa hivi sasa wananchi hao wanaendelea kuteketeza 
nyumba za Askari Polisi hao zilizopo jirani na kituo hicho, licha ya 
Polisi kuendelea kufanya juhudi za kuwatawanya kwa mabomu katika eneo 
hilo.
Aidha
 wananchi hao wameanza kufunga barabara kuu ya Kilwa iendayo Mikoa ya 
Kusini, Lindi na Mtwara kwa mawe, magogo na kuchoma matairi ikiwa ni 
umbali wa kama kilometa moja kutoka kituo cha Polisi Kibiti.
Hali
 inaelezwa kuwa inazidi kuwa tete huku Polisi wa Kibiti wakiendelea na 
jitihada za kudhibiti hali hiyo kwa kufyatua mabomu hewani kujaribu 
kutawanya umati huo wa watu.  Vurugu zinaendelea, Habari kwa hisani ya 
Father Kidevu.
 
 
No comments:
Post a Comment