Wakiwa katika picha ya pamoja watoto ambao ni mapacha watatu, Rehema, Amani na Neema.
 Na Kalisa Kachuchu wa Kajunason Blog, Dar es Salaam.
Mkazi
 wa Kimara, jijini Dar es Salaam, Edwin Rweyongeza, amewaomba Watanzania
 kumsaidia kuwatunza watoto wake mapacha watatu ili waweze kukua vizuri 
kutokana na matatizo ya kipato yanayomkabiri.
Rweyongeza,
 aliitaja misaada hiyo kuwa ni pamoja na Chakula cha watoto lishe, 
yakiwamo maziwa pamoja na matibabu ya kuishiwa na damu yanayoendelea 
kuwa tatizo kwa watoto wake.
Akizungumza
 muda mfupi uliopita na Habari na Matukio Blog, Rweyongeza alisema 
ukosefu wa kipato unaomsumbua, unamfanya ashindwe kuwamudu watoto hao 
waliozaliwa Julai sita mwaka 2011 katika Hospitali ya Mwananyamala.
Alisema
 kutokana na ukosefu wake wa kipato, Ustawi wa Jamii wilaya ya 
Kinondoni, ilikubali Rweyongeza apate msaada kutoka kwa jamii, kwa barua
 yao waliyoandikaa Septemba 14, mwaka 2011 yenye kumbukumbu namba 
W/WG/2011 na kusainiwa na A.Mbusa.
“Naomba
 msaada kutoka kwa Watanzania wenzangu na Dunia kwa ujumla ili watoto 
wangu waweze kupata lishe na kufanikisha maisha yao, maana mimi baba yao
 kwa sasa sina kipato chochote kwasababu sina kazi ya kuniingizia 
kipato.
“Kama
 ningekuwa na uwezo nisingeomba msaada, ukizingatia kwamba watoto watatu
 kuwalea ni kazi kubwa, hasa kwa masuala ya lishe na matibabu, kama vile
 maziwa na mengineyo yanayochangia kukua vizuri,” alisema Rweyongeza.
Kwa
 wenye moyo nahitaji la kumsadia, kijana huyo mwenye miaka 29, alizitaja
 namba zake ni 0767 646599, 0719 909085, huku akitanguliza shukrani zake
 za dhati kwa Watanzania wote.
 Mkazi wa Kimara, jijini Dar es Salaam, Edwin Rweyongeza akiwa na familia yake kwa ujumla.
 
 

No comments:
Post a Comment