Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Wednesday, May 21, 2014

TAPELI SUGU LATIWA MBARONI NJE YA VIWANJA VYA BUNGE-DODOMA

ta3
Tapeli Sugu aliyejulikana kwa Jina la Ally Mwinyi Kutoka Vikindu-Pwani aliyekamatwa Parking za Madereva wa Wabunge-Dodoma akiwa chini ya Ulinzi tayari kwa Kupelekwa Kituo cha Polisi kwa hatua za Kisheria.

ta2Akificha Uso wake asipigwe Picha na Mtambo wetu wa Habari.
ta1
 Tapeli huyu amekuwa akidanganya Madereva wa Wabunge kuwa yeye ni Dereva wa TASAF amekwama Dodoma anahitaji Msaada wa Kifedha,Amekuwa akioneakana Viwanja nje ya Bunge tangu Bunge la Katiba akiwalaghai Watu Mbalimbali kuwa yeye ni Dreva na wakati Mwingine akihusika na Utapeli wa Kujiita Dalali wa Viwanja hapa Dodoma.
ta6
Akiwa Chini ya Ulinzi Mkali.
ta4 ta5Akipandishwa kwenye Gari la Polisi kupelekwa Kituoni kwa hatua zaidi za Kisheria.

Kijana Mmoja aliyefahamika kwa jina la Ally Mwinyi na Kujitambulisha anatokea VIKINDU-Pwani amekamatwa na Jeshi la polisi kwa Ushirikiano na Madreva wa Wabunge hapa Dodoma kwa tabia yake Mbaya ya Kutapeli watu.

Kijana huyo amekuwa akijihusisha na Matukio Mbalimbali ya Utapeli hapa Dodoma kwa nyakati tofauti na kwanji tofauti na kwa watu tofauti.

Utapeli wake amekua akiufanya kwenye Uuzaji wa Viwanja akijidai yeye ni Dalali wa Viwanja,Pia amekamatwa akiwa na Fungo “FAKE” za Gari ambazo amekuwa akitumia kutembea nazo na kujidai yeye ni Dreva wa TASAF amekwama Dodoma hivyo anahitaji Msaada,Kwa nyakati tofauti Madreva wamekuwa wakikutana naye na kuwaomba masaada na hatimaye Kupewa fedha za Kumuwezesha Kurudi Dsm alikosema ndio anafanya kazi ya TASAF.
 
Lakini hadi jana anakamatwa akiwa kwenye jaribio la Kumtapeli Dreva wa Mh:Makongoro Mahanga, ameshadanganya Madreva Wengi na bado amekuwa akionekana  Dodoma tofauti na maelezo yake kuwa anahitaji msaada wa Nauli arejee Dsm tangu Bunge la Katiba Kuanza,Pia ameshukiwa kutapeli watu wengi fedha likiwamo jaribio la Kuiba pikipiki eneo la Kituo cha Polisi Dodoma.

Wakati anakamatwa kulijitokeza watu mbalimbali waliopata kukutana naye na kutapeliwa,Hivyo jeshi la Polisi limemkamata na kumpeleka kituoni kwa hatua zaidi za Kisheria.

Rai,Kama Umetapeliwa  Dodoma,tafadhali fika Kituo cha Polisi Dodoma Mjini kwa msaada zaidi.

No comments: