"Hii gari ilikuwa inatiokea Bugarika inashuka kuelekea mjini, kwa spidi aliyokuwa nayo dereva kwa kweli ilikuwa hairidhishi kwani gari liliyumba kabla ya kufika eneo la Bar ya Bugando Hill, imagine sisi tulikuwa pembeni ya barabara lakini kwa hofu tukalipisha tukakaa pembeni kabisaa. Lilipofika karibu na Shule ya msingi Bugando dereva wa gari kona ikawa kama imemshinda akakwepa akaenda kugonga nguzo ya umeme akawa anahangaika kurudi barabarani eneo ambako kuna kama kivuko kwa wanafunzi ikamshinda na kupitia watoto wawili waliokuwa wakisubiri kuvuka barabara kisha akagota kwenye mawe yaliyopangwa pembezoni" alisema Joseph Nyanda Karumbeti almaarufu kwa jina Baba Teresa, shuhuda wa ajali hiyo.
TUNAOMBA RADHI KWA PICHA ZIFUATAZO
Baadhi ya abiria waliopata majeraha kwenye daladala iliyosababisha ajali wamepelekwa hospitali ya Bugando kupatiwa matibabu.
Mwenyezi Mungu zilaze pema peponi roho za marehemu.
Amen.
No comments:
Post a Comment