Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Thursday, May 15, 2014

HATARI: JENGO LAPOROMOKA HUKO ZANZIBAR, TAZAMA PICHA ZOTE HAPA




Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akijumuika pamoja na baadhi ya wananchi kuangalia athari iliyojichomoza kwenye nyumba ya Bwana Salim Ahmed Salim baada ya ukuta na dari yake kuanguka saa sita usiku juzi mkabala na Skuli ya Sekondari ya Tumekuja Mtaa wa Vuga Mjini Zanzibar.

Athari ya nyumba iliyobomoka hapo Mtaa wa Vuga ilisababisha usumbufu wa watumiaji wa Bara bara itokayo Vuga kuelekea Shangani au Serena na kulazimika kufungwa kwa bara bara hiyo..(Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ).
---------
Mamlaka ya Hifadhi ya Mji Mkongwe wa Zanzibar, Jeshi la Polisi pamoja na Mamlaka ya Usafiri zimekumbushwa kuendelea kuzuia uingiaji wa gari kubwa zenye uzito wa zaidi ya Tani Mbili katika eneo la Mji Mkongwe ili kunusuru majengo yaliyono ndani ya mamlaka hiyo.

Kumbusho hilo limetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipofanya ziara fupi kukagua athari ya nyumba iliyoporomoka ukuta na Dari yake juzi usiku iliyopo Mkabala na Skuli ya Sekondari ya Tumekuja Mtaa wa Vuga Mjini Zanzibar.

Balozi Seif alisema ukaidi wa baadhi ya madereva wa gari kubwa kupitisha Gari gari zao katika eneo hilo umesababisha uchafuzi wa mandhari na haiba ya Mji mkongwe wa Zanzibar ambao hivi sasa uko katika urithi wa Kimataifa.

“ Jeshi la Polisi wakati huu litahitajika kuwa na kazi ya ziada katika kuhakikisha agizo lililotolewa na Mamlaka ya Mji Mkongwe wa Zanzibar linatekelezwa ipasavyo “. Alisisitiza Balozi Seif.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akimpa pole Mmiliki wa Nyumba hiyo Bwana Salim Ahmed Salim kwa hasara aliyoipata alimtaka kuwasiliana na Uongozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Mji Mkongwe wa Zanzibar katika juhudi zaujenzi wa nyumba hiyo utakaozingatia mpango halisi wa uhifadhi wa Mji huo.

Akitoa ufafanuzi wa athari nyingi zilizojitokeza ndani ya nyumba za Mji Mkongwe, Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na Utafiti cha Mamlaka ya Hifadhi ya Mji Mkongwe wa Zanzibar Bibi Madina Haji Khamis alisema ujenzi usiozingatia utaalamu wa Mamlaka husika pamoja na upitishwaji wa gari kubwa ndio sababu kubwa za msingi za athari hizo.

Bibi Madina alifahamisha kwamba baadhi ya wamiliki wa nyumba hizo walikuwa wakipandishia kuta wakati wa ujenzi au matengenezo zaidi ya uwezo wa msingi wa nyumba hizo hali inayoleta athari ya mipasuko ya nyumba hizo sambamba na mitetemeko ya gari kubwa zinazopitishwa pembezoni mwa nyumba hizo.

Mapema Mmiliki wa Nyumba hiyo Bwana Salim Ahmed Salim alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kwamba dalili za kuanguka kwa jengo hilo zilijionyesha mapema kutokana na kuvimba na baadaye kupasukwa kwa eneo la mbele la ukuta wa nyumba hiyo.
Bwana Salim alifahamisha kwamba kutokana na hali hiyo alilazimika kuuarifu Uongozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Mji Mkongwe wa Zanzibar uliolazimia baadaye kwa kushirikiana na jeshi la Polisi kuchukuwa hatua za kuifunga bara bara hiyo.

“ Nilijaribu kuufuata Uongozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Mji Mkongwe uniruhusu kuifanyia matengenezo makubwa nyumba yangu ili baadaye niitumie kwa makazi na familia nyangu lakini bado sijapata jibu na huku inaporomoka “. Alieleza Bwana Salim Ahmed Salim.
Nyumba hiyo ya ghorofa moja mpaka inaporomoka ukuta na dari yake majira ya saa sita juzi usiku lakini hamna watu waliokuwa wakiishi ndani yake.

Mamlaka ya Mji Mkongwe wa Zanzibar kwa kushirikiana na Taasisi nyengine zimelazimika kuzuia Gari zote zinazotumia Bara bara hiyo kutoka Vuga kuingia Shangani au kupitia Serena ili kujaribu kuepuka hatari katika kipindi hichi cha Mvua za Masika.

Kwa mujibu wa hali halisi ilivyo hivi sasa gari zote zinazokusudia kuingia ndani ya eneo la Mamlaka ya Mji Mkongwe zinalazimika kutumia Bara bara itokayo Malindi na zisizidi uzito wa zaidi ya Tani mbili.

Mamlaka ya Hifadhi ya Mji Mkongwe wa Zanzibar kwa miaka kadhaa sasa imo ndani ya Ramani ya Dunia ya urithi wa hifadhi ya Kimataifa chini ya usimamizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu,Sayansi na Utamaduni { UNESCO }.

Wakati huo huo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alikutana kwa mazungumzo na ujumbe wa Kampuni ya uwekezaji vitega uchumi vya sekta za Afya, Kilimo, Umeme, viwanda vidogo vya mazao ya Baharini ya Lucky Exports kutoka Nchini India.

Kampuni hiyo ambayo imefungua Matawi yake katika mataifa mbali mbali Barani Afrika tayari imeshapata usajili wa kufungua Tawi lake Nchini Tanzania.

Katika mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mtaa wa Vuga Mjini Zanzibar Meneja wa Kampuni hiyo Bwana Ravi Rai alisema Taasisi yake imelenga kutoa huduma za afya pamoja na viwanda vidogo vidogo vya mazao ya Baharini.

Bwana Ravi Rai alisema wakati Uongozi wa Taasisi yake ukisubiri kuanza na hatimae kukamilisha taratibu zote za uwekezaji uwekaji wa miradi hiyo umekusudia kusaidia kutoa ajira kubwa kwa wazalendo pamoja na kuongeza mapato ya Taifa.

Alifahamisha kwamba utafiti wa wataalamu wa Taasisi hiyo utafanywa ili kuangalia miradi ambayo kampuni hiyo inaweza kuiwekeza hapa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

“ Tunafarajika kuona kwamba miradi yoyote tutakayoamuwa kuitekeleza kwenye uwekezaji wa mataifa mbali mbali duniani na hasa tukilenga zaidi Bara la Afrika inafadhiliwa na Serikali ya India “. Alisema Meneja huyo wa Lucky Exports.

Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema miradi iliyofikiriwa kuanzishwa na Uongozi wa Kampuni hiyo hapa Zanzibar ya Sekta ya Afya na Viwanda Vidogo vidogo vya mazao ya Baharini itasaidia kustawisha maisha naustawi wa Jamii Nchini.

Balozi Seif aliuagiza Uongozi wa Kampuni hiyo ya Lucky Exports kutoka Nchini India kurahisisha maombi yao ya uwekezaji ili taasisi zinazohusika na uwekezaji ziweze kuyapitia na kutoa maamuzi yanayostahiki kwa wakati muwafaka.

Kampuni ya Uwekezaji ya Lucky Exports ya Nchini India ambayo tayari imeshafungua matawi yake katika Mataifa ya Ethiopia, Guinea Bisau, Malawi na Tanzania inajihusisha zaidi na uwekezaji wa miradi y

No comments: