
Muigizaji marufu wa filamu barani Afrika AKI amevunja ukapela na kuchua jiko aka mke tayari kuanza safari ya ndoa katika maisha yake.
Aki amejizolea umaarufu mkubwa kutokana na umbo lake na umahiri wake katika tasnia ya filamu duniani. 

Mambo yalikuwa hivi .
BREKING NEWS: JK ATIA SAINI MUSWADA WA SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
leo, Jumanne, Novemba 29, 2011, ametia saini Muswada wa Sheria ya
Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011.
Hatua hiyo ya Mheshimiwa Rais kutia saini Muswada huo inakamilisha safari
ya kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 baada ya Bunge
kuwa limepitisha Muswada huo uliowasilishwa na Serikali katika kikao
kilichopita cha Bunge.
Aidha, kutiwa saini kwa Muswada huo ili uwe Sheria ni hatua kubwa na muhimu
katika
 safari ya kutungwa kwa Katiba mpya ya Tanzania kama ilivyoahidiwa 
na Mheshimiwa Rais Kikwete katika salamu zake za Mwaka Mpya kwa 
wananchi Desemba 31, mwaka jana, 2010.
Pamoja na kutiwa saini hiyo bado Serikali itaendelea kusikiliza maoni na
mawazo ya wadau na wananchi mbalimbali kuhusu namna ya kuboresha sheria hiyo.
Hivyo, Mheshimiwa Rais Kikwete anatoa wito kwa mwananchi yoyote mwenye
maoni ama mawazo ya namna ya kuboresha Sheria hiyo, ajisikie yuko huru
kutoa maoni yake na Serikali itasilikiza na kuchukua hatua zipasazo.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
29 Novemba, 2011.
 HATIMAE
 KILIMANJARO STARS IMEFANIKIWA KUPATA USHINDI WA KWANZA KWENYE 
MASHINDANO YA CECAFA TUSKER CHALLENGE CUP 2011 BAADA YA KUIFUNGA 
DJIBOUTI MABAO 3-0.
 HATIMAE
 KILIMANJARO STARS IMEFANIKIWA KUPATA USHINDI WA KWANZA KWENYE 
MASHINDANO YA CECAFA TUSKER CHALLENGE CUP 2011 BAADA YA KUIFUNGA 
DJIBOUTI MABAO 3-0.
MABAO HAYO YAMEFUNGWA NA THOMAS ULIMWENGU,MWINYI KAZIMOTO NA YUSUF RASHID.
WAKATI HUO HUO RWANDA IMEIFUNGA ZIMBABWE MABAO 2-0 KWENYE MCHEZO ULIANZA MAPEMA.

KILIMANJARO STARS YAITANDIKA DJIBOUTI MABAO 3:0
MABAO HAYO YAMEFUNGWA NA THOMAS ULIMWENGU,MWINYI KAZIMOTO NA YUSUF RASHID.
WAKATI HUO HUO RWANDA IMEIFUNGA ZIMBABWE MABAO 2-0 KWENYE MCHEZO ULIANZA MAPEMA.
SOKO LA KISIMANI MJI MDOGO WA TUNDUMA LILIVYOTEKETEA KWA MOTO.
Soko
 la Kisimani lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba 
mkoani Mbeya limeteketea kwa moto hapo jana kuanzia majira ya Saa 10 
jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka 
yameteketea kwa moto huo. Chanzo hakijaweza kubainishwa lakini inadaiwa 
kuwa Umeme uliporudi baada ya kukatika ndipo moto ulipoanza katikati ya 
Soko hilo 
Vibanda
 vilivyokuwa vimejengwa kwa mbao vimeteketea na kubakia masalia ya 
mabati yaliyotumika kuezekea vibanda hivyo katika Soko la Kisimani 
lililopo mji mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba mkoani Mbeya, 
jana kuanzia majira ya Saa 10 jioni na kusababisha hasara kubwa ambapo 
vibanda vya biashara na maduka yameteketeakwa moto huo. 
Magari
 ya kampuni ya Ujenzi wa barabara ya Tunduma mpaka Sumbawanga yalifika 
kutoa msaada wa kudibiti moto katika  Soko la Kisimani lililopo mji 
mdogo wa Tunduma, wilaya ya mpya ya Momba  mkoani Mbeya lililoteketea 
kwa moto hapo jana kuanzia majira ya Saa 10  jioni na kusababisha hasara
 kubwa ambapo vibanda vya biashara na maduka  yaliteketea
Mzee
 huyu alishikwa na bumbuwazi la kutoamini duka lake likiteketea kwa moto
 ambapo hivi karibuni aliingiza mzingo wa bidhaa kutoka jijini Dar es 
salaam uliogharimu shilingi milioni Ishirini 
 
No comments:
Post a Comment