Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Tuesday, November 15, 2011

WABUNGE KUJIACHIA NA MAMISS UTALII VYUO VIKUU


Waheshimiwa wabunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania, ni miongoni mwa wageni waalikwa katika shindano la kuwania taji la Vipaji la Miss Utalii Vyuo Vikuu 2011/12 – KANDA YA KATI.
Shindano hilo la awali litafanyika katika ukumbi wa kisasa na maalufu mkoani Dodoma wa CLUB 84, kabla ya fainali kuu ya Miss Utalii vyuo Vikuu 2011/12 – KANDA YA KATI zi
takazofanyika sambamba na sherehe za miaka 50 ya Uhuru tarehe 9-12-2011.
Jumla ya warembo 25 kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM),Chuo kikuu Cha ST John’s ,Chuo cha Mipango,na Chuo cha Biashara (CBE) watapanda jukwaani kuwania taji la Miss Utalii Vyuo Vikuu 2011/12 VIPAJI – Kanda ya kati. Warembo wote watapanda jukwaani kuwania taji hilo kwa kushindana kucheza na kuimba nyimbo na ngoma za asili za makabila ya Tanzania,pia wataPita jukwaani katika mavazi ya asili na ubunifu.
Hii itakuwa ni fulsa ya pekee kwa waheshimiwa wabunge na wakazi wa Dodoma na mikoa ya jirani,kushudia jinsi warembo wasomi wa vyuo vikuu wakidumisha utamaduni wa mtanzania kwa kucheza na kimba nyimbo na ngoma za asili ya makabila ya mtanzania.
Wadhaminiwa ni LAKAIRO HOTEL (Mwanza) Royal Village Hotel, NAM Hotel, KITOLI Hotel, Happy Fashion, Shabiby Bus Services, New Soft Hair Dressing Saloon, Becko Quality Center, CF communication ,Book Center and Stationary, Hotel Kitemba, CLUB 84, Master Pub, Musa transport, Perugina Investment, Dar city Collage,Father  Kidevu Blog, shaabanmpalule.blogspot.com,michuzijr.blogspot.com,Clouds FM,misstourismtanzania.blogspot.com,misstourismorganisation.blogspot.com,PAPA Msofe na Tambaza Auction Mart & General Broker,Asaah Salon.
 Majina ya washiriki wa shindano hilo linalo.Esther Maganza (Udom),Getrude Avelyn(Mipango),Loveness Shore(Mipango),Lisa Jackson(Mipango) ,Lilian Maleo(Udom),Alphonca Victor(Mipango),Irine Richard(Cbe),Jennifer Mafuru(Udom),Hawa Nyange(Udom),Lilian Charles(Mipango),Sarah Charles(Mipango),Violeth Ndawi(Mipango),Irine Julius(Mipango),Juster Julius(Mipango),Anneth Swai(St.John),Anitha Charles (Udom),Jacquiliney Kinabo(Udom),Pricilla Mponeja(Udom) wa fainali hizo watawakilisha Vyuo Vikuu vya kanda ya kati katika fainali za taifa za Mis Utalii Tanzania 2011/12 zitakazo fanyika Februari 2012.
Kambi a mazoezi ya warembo hao inaendelea katika hoteli ya kitalii ya Royal village hotel Dodoma,chini ya walimu wa Mariam Hamis (Miss Ualii Dodoma 2010/11na Jamida Abdul ( Miss utlii kigoma 2010/11) . haki katika kambi ya mazoezi ni ya ushindani mkubwa kutokana na washiriki wa kila chuo kudhamiria kutwaa taji la Vipaji hapo tarehe 18-11-2011na taji lenywe la MissUtalii Vyuo Vikuu 2011/12 – kanda ya Kati hapo tareh 9-12-2011. 



J-LO SASA ANATOKA NA DANCER WAKE 

Jennifer Lopez has officially moved on from ex-husband Marc Anthony and is now dating 24-year-old background dancer Casper Smart
 

CHADEMA NA NCCR WAPINGA KUBURUZWA BUNGENI
WABUNGE wa Chadema na NCCR-Mageuzi jana walilitikisa Bunge baada ya kuungana kutoka nje ya ukumbi kupinga kile walichodai kuwa ni Spika wa Bunge, Anne Makinda kuwadharau kwa kuwanyima haki zao kwa mujibu wa kanuni.Wakati wabunge hao wakitoka bungeni kugomea muswada huo, Chama cha Majaji Wastaafu Tanzania (Tarja), kimetoa tamko kupinga hadidu za rejea za tume itakayoratibu mchakato wa kuundwa kwa Katiba Mpya kutolewa na Rais. Licha ya Spika Makinda kuukingia kifua muswada huo katika utangulizi wake kabla ya kuruhusu uwasilishaji wa hoja kwa pande zote akisema ulifuata kanuni za Bunge, haikusaidia kwani muda mfupi baada ya Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria, Tundu Lissu kutoa maoni ya Kambi ya Upinzani, wabunge hao waliamua kuondoka. Muswada huo wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2011, ambao uliwasilishwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani umepata pia upinzani kutoka kwa wanaharakati nchini ambao wametishia kufanya maandamano nchi nzima endapo wabunge watauridhia. 



Anaweza kuwa na miaka 6 tu lakini Cruz Beckham tayari ameshaanza kufuata nyayo za baba yake.

Cruz tayari ameshaanza kucheza soka lakini inaonekana tayari ameshaanza kufuata mitindo ya nywele ya zamani ya mzazi wake.
Cruz alionekana jana akiwa anacheza soka huku kichwani akiwa kanyoa mtindo wa “kiduku” ambao Beckham alinyoa miaka 10 iliyopita

Mtoto huyo mdogo kabisa wa kiume wa Beckham, pia style yake ya nywele imeonekana kufanana na na style ya Roberto De Niro katika filamu ya Taxi Driver.
Cruz pia anajulikana kwa kupenda kuchora temporarly tattos – kitu kingine ambacho amekiiga kutoka baba yake.
Alionekana na baba yake mjini LA akiwa anachorwa katika painting session at Color Me Mine – sehemu ambayo watoto wanajifunza kuchora kwa ubunifu wao wenyewe.
 

MAFURIKO UWANJA WA NDEGE MWANZA YASABABISHA UWANJA KUFUNGWA KWA MUDA, ABIRIA WASHINDWA KUSAFIRI

Mvua kubwa iliyonyesha leo jijini Mwanza kwa takribani masaa manne imeathiri kwa kiasi kikubwa shughuli za usafiri na usafirishaji kwa njia ya anga.
Hali halisi....hatoki mtu...!!
kwasababu za kiusalama hakuna ndege iliyoruhusiwa kutoka au kuingia Air port Mwanza.
Hali ilikuwa mbaya zaidi majira ya saa mbili asubuhi ambapo maji mengi yaliyokuwa yakitiririka kutoka eneo la mwinuko kaskazini mwa kiwanja cha ndege Mwanza, yalisababisha taswira ya uwanja kubadilika na kuwa kama sehemu ya mto mkubwa unaotiririsha maji kuelekea ziwa victoria.
Pichani ni kama ndege iliyogota katikati ya shamba la mpunga kumbe laaa!! ni ndege iliyo katika eneo stahiki la maegesho ya ndege.
Wafanyakazi mbalimbali kiwanjani hapo wakishughulika kusafisha njia za ndege mara baada ya magugu na tope jingi kutanda eneo hilo.
Chekshia ngazi za ndege....
Wafanyakazi wa idara tofauti kiwanjani hapo wakihaha kuzima swichi za umeme kiwanjani hapo mara baada ya kina cha maji kuanza kupanda taratibu kikitishia usalama.
Wafanyakazi sekta ya mizigo walifanya kazi ya ziada kunusuru mizigo ilokuwa tayari imepakiwa kitengo cha mizigo isilowe.
Mara baada ya maji kupungua unaweza kuona jinsi miundo mbinu hasa njia za ndege ilivyoathirika. 


 KIM KARDASHIAN  KUSHITAKIWA
Kim Kardashian
In a new legal move, a competing hair removal company claims Kim Kardashian and the company she works for have misled consumers about all things follicle.

Kim is the hairless face of TRIA, a home laser hair-removal system. Radiant, a rival company that sells no!no! hair, claims Kim has deceived the public with her pitch, specifically ...

-- Kim claims she uses TRIA over her entire body, but Radiant maintains even TRIA says it's not safe for the face, head, ears, neck, nipples, genitals or anus.

-- Kim touts TRIA by claiming "You'll never need razors or shaving cream again."  But according to the lawsuit, TRIA's instructions note the product is supposed to be used in concert with shaving.

-- Kim has said numerous times she's been getting professional hair removal treatments for more than a decade, so Radiant wants to know how she can possibly say TRIA is her secret.

Radiant wants TRIA and Kim to stop making the alleged false claims ... and is seeking unspecified damages.

No comments: