Mheshimiwa
 Mbunge wa jimbo la Mbeya mjini Bwana Joseph Mbilinyi akiwasihi wananchi
 kuwa watulivu na kwamba mgogoro umekwisha na utatuliwe kisayansi badala
 ya kisiasa na pia amewapongeza machinga kwa utulivu waliouonesha bila 
kupora bidhaa madukani.
 Halaiki
 ya wananchi waliofika kuusikiliza mustakabali wa wafanyabiashara 
wadogowadogo maarufu kama machinga kuendelea na biashara zao katika 
maeneo yao ya awali, wakati utaratibu wa maeneo ya kufanyia biashara 
ukiandaliwa na halmashauri ya jiji la Mbeya.
Maelfu
 ya wananchi waliofika kuusikiliza mustakabali wa wafanyabiashara 
wadogowadogo maarufu kama machinga kuendelea na biashara zao katika 
maeneo yao ya awali, wakati utaratibu ukiandaliwa na halmashauri ya jiji
 la Mbeya.
 Jeshi
 la Wananchi Tanzania(JWTZ), likiwasaidia Jeshi la Polisi kuweka hali ya
 amani na utulivu mara baada ya kuisha kwa mkutano uliofanyika katika 
kituo cha mabasi madogo ya abiria(daladala) eneo la Kabwe Mwanjelwa 
jijini Mbeya
Wananchi
 wakirudi makwao kwa furaha baada ya mgogoro uliodumu kwa siku mbili 
kumalizika, baada ya hotuba ya Mheshimiwa mbunge wa jimbo la Mbeya mjini
 Bwana Joseph Mbilinyi.
 
 
No comments:
Post a Comment