Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Sunday, November 20, 2011

UDOM YASHINDA REDDS UNI FASHION 2011


  Baadhi ya washiriki wa shindano la mitindo lililojulikana kama Uni Fashion Bash kutoka vyuo mbalimbali vya mjini Dodoma wakicheza wakati wa utambulisho lililofanyika Royal Village Dodoma jana.
  Baadhi ya washiriki wa shindano la mitindo lililojulikana kwa Uni Fashion Bash kutoka vyuo mbalimbali vya mjini Dodoma wakicheza wakati wa utambulisho wa shindano hilo lililofanyika kwenye ukumbi wa Royal Village mjini Dodoma jana.
  Mshindi wa kwanza wa shindano la wanamitindo lililojulikana kama 'Uni Fashion Bash',Respicious Denis (kushoto)kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) akipokea zawadi yake ya shilingi laki tano kutoka kwa mwakilishi wa TBL kanda ya kati John Tesha, baada ya kutangazwa mshindi katika shindano hilo lililofanyika ukumbi wa Royal Village mjini Dodoma jana.
  Baadhi ya washiriki wa shindano la ubunifuwa mavazi lililojulikana kwa Uni Fashion Bash kutoka vyuo mbalimbali vya mjini Dodoma wakitambulishwa jukwaani wakati wa shindano hilo.
  Mshindi wa kwanza wa ubunifu wa mavazi wa shindano la 'UNI fashion Bash' ,Irene Rwakatale (kushoto) akipokea akipokea zawadi yake ya shilingi laki saba kutoka kwa Meneja wa Redds, Victoria baada ya kutangazwa mshindi wa shindano hilo jana.
  Baadhi ya wanafunzi kutoka vyuo malimbali vya mjini Dodoma wakishangilia wakati wa shindano hilo.
  Baadhi ya wanafunzi kutoka vyuo malimbali vya mjini Dodoma wakishangilia wakati wa shindano hilo.
  Mwanamuziki wa kizazi kipya, Mwana FA, akishambilia jukwaa wakati wa shindano hilo.
Mwana FA, akipagawisha na mmoja wa shabiki wake jukwaani wakati wa onyesho hilo.

KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager imetangaza rasmi kufutwa kwa mashindano ya 'ALL AFRICA CUP 2011-BLANTYRE- MALAWI' yaliyotarajiwa kuanza Novemba  22, hadi 26, 2011. 

 Akitangaza mabadiliko ya safari hiyo, Meneja wa bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo, alisema kuwa Pamoja na mashindano hayo kufutwa Bia ya Safari, imeandaa ziara ya timu ya Taifa ya Pool katika mikoa ifuatayo ya Dodoma, Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga baada ya kushauriana na chama cha mchezo huo ili kuwafanya wachezaji wa timu ya taifa kuwa katika hali ya mchezo na kufanya mazoezi baada ya kuahirishwa kwa mashindano hayo yaliyokuwa yafanyike Malawi.

Aidha imeelezwa kuwa kuahirishwa kwa mashindano hayo kufanyika Malawi kumefuatia kutokea kwa machafuko ya Kisiasa na hii itatoa nafasi kwa mikoa iliyotajwa kuiona timu yao ya Taifa na baadhi ya wachezaji wakali wa mikoa hiyo kupata nafasi ya kucheza na wachezaji wa timu yhiyo ya Taifa.

RAIS JAKAYA M. KIKWETE ATUA DODOMA RASMI KUHUDHURIA VIKAO VYA CHAMA CHAKE CCM.

Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Jumamosi (Nov 19) jioni amewasili mjini Dodoma tayari kwa vikao muhimu vya chama hicho tawala vitavyofanyika kwa siku nne katika ukumbi wa Makao Makuu ya CCM maarufu kama White House.
Katika Uwanja wa ndege wa Dodoma Dkt Kikwete amepokewa na viongozi pamoja na wana CCM wengi wakiongozwa na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilal na Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye ni Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM.
Na Mwandishi Maalum, Dodoma, Jumamosi Nov. 19, 2011.
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mbunge wa CHADEMA John Shibuda katikati ni Mzee Pius Msekwa. 

MASHINDANO YA NGUMI YA KOVA CUP YAMALIZIKA

Bondia Mussa Mohamedi (kulia) akimfulumusha makonde mfululizo, Fadhili Hassani wakati wa mpambano wa mashindano ya Kova Cup yaliyomalizika, Dar es salaam jana Mussa alishinda kwa K,O ya raundi ya tatu.

No comments: