Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Thursday, November 17, 2011

WANAFUNZI 22 KUANGUKIWA NA JUMBA BOVU UDSM

  Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Yunus Mgaya, amesema wanafunzi 22 waliosimamishwa, wanaandaliwa mashtaka kuhusiana na matukio yaliyosababisha vurugu chuoni hapo.
 Akizungumza n jana jijini Dar es Salaam, Profesa Mgaya alisema mashitaka hayo yatakamilika ndani ya wiki hii. 
 Alisema wanafunzi hao watapewa siku saba za kujitetea na baada ya hapo itaundwa kamati ya nidhamu ya wanafunzi ili kusikiliza utetezi wao. Profesa Mgaya alisema chuo hakijawafukuza wanafunzi na kwamba, katika suala hilo kuna taratibu mbalimbali, ambazo zinatakiwa kufuatwa.
 Hata hivyo, Profesa Mgaya alisema baada ya utetezi wao kusikilizwa, itaandikwa ripoti, ambayo itakuwa na mapendekezo yatakayotumika katika kutoa maamuzi. 
 Alisema kila mwanafunzi atapewa adhabu kulingana na mashitaka. 
 Profesa Mgaya alisema wanafunzi 50, ambao wamefikishwa mahakamani, watano kati yao, tayari walishasimamishwa, hivyo watakuwa wanakabiliwa na adhabu mbili.


Amar’e Stoudemire and Fabolous turned up the swagu last night as they celebrated their birthdays together at the Catch Roof in New York. The fellas got dapper as they celebrated with celebrity friends Adrienne Bailon, Emily B, Rosci Diaz, Jessica White, Angela Simmons, Trey Songz, Ryan Leslie and plenty more.

 MWALIMU APIGWA HADI KUFA
Mkuu wa shule Noko Moabelo
Raia mmoja wa Afrika kusini ameshtakiwa kwa mauaji baada ya kaka yake kupigwa hadi kufa mbele ya wanafunzi wake karibu na mji wa Polokwane kaskazini mwa nchi hiyo.
Guilford Shapo, mwalimu katika shule ya msingi ya Masehlong, alishambuliwa alipokuwa akisimamia mitihani siku ya Jumanne, chombo cha habari cha umma cha Afrika kusini kiliripoti.
Mdogo wake wa kiume Happy Shapo ameshtakiwa kwa uhalifu huo, msemaji wa polisi Ronel Otto aliiambia BBC.
Bw Shapo hakutakiwa kusema lolote na kesi hiyo imeahirishwa hadi wiki ijayo.
Gazeti la nchi hiyo la Star lilimnukuu Noko Moabelo, mkuu wa shule katika kijiji cha Ga-Mmasehlong kwenye jimbo la Limpopo akisema, " Tulishtushwa na wanafunzi walipopiga kelele na kukimbia kutoka darasani."
Alisema, "Bw Shapo alikuwa mwalimu pekee wa kiume katika shule hiyo. Tukiwa wanawake, hakuna hata mmoja wetu ambaye angeweza kujaribu kupambana na mshukiwa huyo."
Majirani waliosikia makelele hayo walikimbilia shuleni hapo kusimamisha mashambulio hayo ya mapanga, gazeti hili liliripoti.
Guilford Shapo alifariki dunia baadae kutokana na majeraha.
Luteni Kanali Otto alisema ombi lake la dhamana litasikilizwa Novemba 21 siku ya Jumatatu.
Idadi ya matukio ya mauaji yamepungua sana Afrika kusini tangu kumalizika kwa enzi za ubaguzi wa rangi mwaka 1994, lakini bado matukio hayo yanaongoza ukilinganisha na nchi nyingine baada ya kutokea zaidi ya mauaji ya watu 40 kwa siku.

No comments: