Rais
 Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa shindano la
 kumsaka Miss Utalii wa Dunia mwaka 2006 mara walipomtembelea IKULU 
(Picha na Maktaba ya Miss Utalii ORG.
Rais Kikwete akiwa na Gideon Chipungahelo (Chips)
Tanzania
 kwa mara nyingine tena imepewa heshima ya kuwa wenyeji wa fainali za 
Dunia za Miss Utalii ,ambapo safari hii , Kamati ya Dunia ya Miss 
Tourism United Nation Organisation, imeipa heshima ya kuwa wenyeji wa 
shindano la Miss tourism United Nations World 2012. 
Kupitia
 kampuni ya Miss Tourism Tanzania Organization, waandaaji wa mashindano 
ya Miss Utalii Tanzania, Tanzania imezishinda nchi nyingine nne zilizo 
kuwa zikiwania fulsa hiyo adimu, nchi hizo ni pamoja na Jamaica, 
Korea,China,Kenya na Nigeria. 
Sambamba
 na uteuzi huo, kamati hiyo ya Dunia imemteua Gideon E.G.chipungahelo 
kuwa mkurugenzi wa mashindano hayo barani afrika , na makamu wa rais wa 
mashindano hayo Duniani .kuanzia Novemba 1,2011. 
Mashindano
 hayo yatashirikisha jumla ya nchi 120, duniani, na kurushwa LIVE katika
 TV za nchi zaidi 100 duniani kote. Pamoja na washiri hao,waandishi wa 
habari kutoka nchi zaidi 70 , vipngozi zaidi 120 na wanafamilia zaidi 
200 wanatarajiwa kuja nchini sambamba na washiriki wa mashindano hayo. 
Tuna mshukuru mungu kwa kuweza kushinda nafasi na heshima hii kwa nchi 
yetu, hasa katika wakati huu ambapo ushindani katika sekta ya utalii na 
uwekezaji baina ya nchi na hata baina ya mabara ni mkubwa. Tunajisikia 
ufahari kwa nchi yetu na kuwa sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali 
katika kutangaza utalii,utamaduni na mianya ya uwekezaji wa Tanzania 
kitaifa na kimataifa. Shindano hili litatyoa fulsa ya pekee kwa Tanzania
 ,kutangaza utalii,utamaduni na mianya ya uwekezaji kimataifa na hata 
kitaifa,pia kuuthibitishia ulimwengu kuwa vivutio vikuu vya utalii 
Afrika ikiwemo Mlima Kilimanjaro,Ngorongoro Creators na Serengeti vipo 
Tanzania. Hii ni fulsa pia kwa viwanda na bidhaa za Tanzania kujitangaza
 kimataifa na kuingia katika masoko ya kimataifa. 
Taratibu
 zote za mikataba za kimataifa zimekamilika,tunatarajia kutangaza rasmi 
tarehe ya kufanyika kwa shindano hilo nchi, wakati wa fainali za Miss 
Utalii Vyuo Vikuu 2011/12 – Kanda ya kati, litakalo fanyika Ijumaa , 
tarehe 30-12-2011 katika ukumbi wa Club la Azziz Dodoma. Shindano hilo 
linashirikisha zaidi ya warembo 15 kutika vyuo vikuu vilivyopo katika 
mikoa ya kanda ya kati, ikiwemo mikoa ya Dodoma, Singida na Tabora. 
Tayari
 taratibu za kitaifa zimanza kufanywa ,zikiwemo za kushirikisha wadau na
 mamlaka mbalimbali wa ndani na nje ya nchi. Hatua zote madhubuti 
zimechukuliwa na zinaendelea kuchukuliwa kwa kuzingatie uzoefu na 
mapungufu ya liyo jitokeza katika fainali za Dunia zilizofanyika nchini 
mwaka 2006,pale Ubungo Plaza 11-3-2006. 
Mkataba
 wa kufanyika kwa fainali hizo za Dunia ,nchini umesainiwa na Rais wa 
Miss Tourism United Nation Organisation, Ngugu Leon Willians na Rais wa 
Miss Tourism Tanzania Organisation ,Gideon Chipungahelo tarehe 
8-12-2011. 
 
 


No comments:
Post a Comment