
Wema na Diamond

Habari zisizo rasmi zilizoenea mjini ni kwamba Wema sepetu amjia juu Jokate baada ya kusemekana alivunja amri ya sita wakati wakifanya video ya "mawazo" na Mchumba wa Wema namzungumzia Diamond.
Nyeti zinaendelea kusema Wema alifumania Jokate akibadilisha radha ya ndimi na Diamond,hata hivyo wema alilalama sana kutokana na kumwamini JOKATE  ni rafiki wa karibu asingeweza kumpa mambo Diamond.
 nyeti zaidi...
KISHINDO
 cha Jokate Mwegelo ni kizito, kimeingia ndani ya uhusiano wa brazameni,
 Naseeb Abdul ‘Diamond’ na Wema Sepetu kisha kuwafanya wawili hao kila 
mmoja kushika hamsini zake.
Wema,
 amefunga virago, ameondoka nyumbani kwa Diamond, Sinza Madukani, Dar es
 Salaam kwa mtindo wa “wanakwenu kwa heri, nimechoka masimango, narudi 
nyumbani kwetu leo.”
Madai
 ‘yanahiti pointi’ kuwa Diamond na Jokate wapo kwenye penzi jipya lenye 
nguvu, Wema ameligundua hilo, ameona ni maji marefu, kwa hiyo amejiweka 
pembeni kuepuka msongamano.
Inazidi kudaiwa kwamba Wema alijaribu kumfanya Diamond atulie lakini ikashindikana, ilipodhihirika Jokate ameshika mpini, alianza kupata mateso ya moyo na hisia kwa jinsi alivyofanywa ‘spea tairi’.
Madai ‘yanahiti’ pia kwamba Wema alithibitisha kuwa Diamond na Jokate 
wanamchezea ‘ukuti ukuti’ baada ya kuwafumania wakiwa ‘vere klozi’ 
kimahaba kwenye Hoteli ya Picolo, Masaki, Dar es Salaam.
Hata hivyo, inadaiwa kuwa Wema alipowakuta Diamond na Jokate, 
hakuangusha varangati kama mmiliki, badala yake alinywea utadhani yeye 
ndiye mwizi kisha akawaambia: “Samahanini sana kwa kuwaingilia kwenye 
starehe zenu.”
WAZIRI NCHIMBI AUNDA KAMATI YA KUPATA VAZI LA TAIFA
WIZARA
 ya Habari, vijana, utamaduni na michezo, imesema mchakato wa kupata 
vazi la taifa unaendelea vizuri kwani wabunifu wazalendo wa mitindo ya 
mavazi nchini wameshirikishwa na kutoa mapendekezo yao.
Taarifa ya waziri wa Habari, vijana, utamaduni na michezo, DOKTA Emmanuel Nchimbi amesema ili kuhitimisha mchakato huo.
 Kamati maalum ya kukamilisha mchakato huo imeundwa ambapo kamati hiyo 
inaongozwa na Mwenyekiti wake JOSEPH KUSAGA, katibu wake ni ANGELA NGOWI.
Wengine
 ni wajumbe ambao ni HABIBU GUNZE, JOYCE MHAVILLE, MUSTAFA HASSANALI, 
ABSALOOM KIBANDA, MAKWAIYA KUHENGA na NDESAMBUKA MERINYO. 
   Itakumbukwa
 kuwa Serikali, kupitia Idara ya Maendeleo ya Utamaduni ya Wizara ya 
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, ilianzisha mchakato wa kupata Vazi
 la Taifa mwaka 2004. 
 
 

No comments:
Post a Comment