Kaimu
 Katibu Mtendaji wa BASATA, Godfrey Lebejo akisisitiza jambo kwenye 
programu ya Jukwaa la Sanaa inayofanyika kila wiki makao makuu ya Baraza
 hilo Ilala Sharif Shamba na kuhudhuriwa na wadau wa Sanaa. Kulia kwake 
ni Afisa Uhusiano wa Uhamiaji Bi. Tatu Burhan. 
Ssp
 Edson Kasekwa kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu, Kitengo maalum cha 
Operesheni uzuiaji uhalifu akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu
 matumizi ya Sanaa katika Polisi Jamii na Ulinzi Shirikishi. Kulia kwake
 ni Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa, BASATA Bi. Vivian Shalua. 
Afisa
 Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji Tatu Burhan akieleza haja ya Jamii 
kushirkiana na Idara yake katika kupambana na tatizo la Uhamiaji haramu 
nchini. Kushoto kwake ni Bw. Lebejo. 
Kikundi
 cha Ngoma cha Jeshi la Polisi kikitumbuiza kwenye Programu ya Jukwaa la
 Sanaa ambapo elimu kuhusu dhana ya Ulinzi Shirikishi na Polisi Jamii 
ilitolewa kwa Wadau zaidi ya 140.
Sehemu ya Maafisa wa Jeshi la Polisi wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye Programu hiyo ya Jukwaa la Sanaa. 
Mkongwe
 wa Sanaa za Maonyesho Mzee Nkwama Bhallanga akielezea masuala 
mbalimbali kuhusu Sanaa Shirikishi katika Polisi Jamii na Ulinzi 
Shirikishi. 
Wadau wa Sanaa wakiifuatilia Programu ya Jukwaa la Sanaa wiki hii.
Baraza
 la Sanaa la Taifa (BASATA) na Jeshi la Polisi nchini wameunda 
kikosikazi maalum kitakachokuwa kikifuatilia uharamia na maovu 
mbalimbali katika shughuli za Sanaa na Burudani.
Kikosikazi
 hicho kimeundwa baada ya Jeshi la Polisi nchini kutumia Sanaa 
shirikishi katika kutoa elimu kwa wadau wa Sanaa kuhusu dhana ya polisi 
jamii na ulinzi shirikishi kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila 
wiki makao makuu ya BASATA Ilala Sharif Shamba.
 
 
 
  
  
  
  
  
  
 
No comments:
Post a Comment