Pages

BRAND NEW MUSIC

metty magese

metty magese

Listen & Download

http://mdundo.com/a/32626

Tuesday, January 31, 2012

WIZI WA KAZI ZA SANAA KISHA KAZI

Kaimu Katibu Mtendaji wa BASATA, Godfrey Lebejo akisisitiza jambo kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa inayofanyika kila wiki makao makuu ya Baraza hilo Ilala Sharif Shamba na kuhudhuriwa na wadau wa Sanaa. Kulia kwake ni Afisa Uhusiano wa Uhamiaji Bi. Tatu Burhan.
Ssp Edson Kasekwa kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu, Kitengo maalum cha Operesheni uzuiaji uhalifu akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu matumizi ya Sanaa katika Polisi Jamii na Ulinzi Shirikishi. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa, BASATA Bi. Vivian Shalua.
Afisa Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji Tatu Burhan akieleza haja ya Jamii kushirkiana na Idara yake katika kupambana na tatizo la Uhamiaji haramu nchini. Kushoto kwake ni Bw. Lebejo.
Kikundi cha Ngoma cha Jeshi la Polisi kikitumbuiza kwenye Programu ya Jukwaa la Sanaa ambapo elimu kuhusu dhana ya Ulinzi Shirikishi na Polisi Jamii ilitolewa kwa Wadau zaidi ya 140.
Sehemu ya Maafisa wa Jeshi la Polisi wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye Programu hiyo ya Jukwaa la Sanaa.
Mkongwe wa Sanaa za Maonyesho Mzee Nkwama Bhallanga akielezea masuala mbalimbali kuhusu Sanaa Shirikishi katika Polisi Jamii na Ulinzi Shirikishi.
Wadau wa Sanaa wakiifuatilia Programu ya Jukwaa la Sanaa wiki hii.

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na Jeshi la Polisi nchini wameunda kikosikazi maalum kitakachokuwa kikifuatilia uharamia na maovu mbalimbali katika shughuli za Sanaa na Burudani.

Kikosikazi hicho kimeundwa baada ya Jeshi la Polisi nchini kutumia Sanaa shirikishi katika kutoa elimu kwa wadau wa Sanaa kuhusu dhana ya polisi jamii na ulinzi shirikishi kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila wiki makao makuu ya BASATA Ilala Sharif Shamba.

No comments: