
UHUSIANO wa kimapenzi, ulioanzishwa kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook, umesababisha kifo cha mrembo nchini Nigeria.
Habari za mtandaoni zinadai kuwa
 mrembo huyo (jina halikutajwa) pamoja na boyfriend wake (jina pia 
halijatajwa), walikuwa kwenye uhusiano wa muda mrefu.
Imedaiwa kuwa wakati wawili hao 
wakiwa kwenye utekelezaji wa hatua za mwanzo za kufunga ndoa, mrembo 
huyo alimtaarifu boyfriend wake kuwa amepata mpenzi mwingine kwa njia ya
 Facebook.
Chanzo cha habari kiliiambia 
tovuti moja ya nchi hiyo kwamba mrembo huyo alianzisha urafiki wa 
Facebook na kijana mmoja raia wa Marekani (jina halijatajwa) kabla ya 
kibao kubadilika na kuwa wapenzi.
Chanzo kiliendelea kupasha 
habari kwamba mrembo huyo na mpenzi wake wa Facebook, walidumisha 
uhusiano wao kwa njia ya mawasiliano ya simu kwa muda mrefu kabla ya 
kukata shauri la kuonana ana kwa ana.
“Yule kijana raia wa Marekani 
alitembelea Nigeria, akafikia hoteli moja kubwa. Yule mrembo akaenda 
kukutana naye na kutumia muda mrefu chumbani.
“Ni kama baada ya kukutana ndiyo
 mapenzi yaliongezeka zaidi, kwani alipoondoka hotelini, yule mrembo 
alirudi kwa boyfriend wake aliyepanga kufunga naye ndoa na kumueleza 
kwamba mapenzi yamekwisha.
“Baada ya kuambiwa hivyo, kijana aliyekuwa na mategemeo ya kufunga ndoa na mrembo huyo, alimpeleleza mpenzi wake na kubaini mahali ambako kijana kutoka Marekani alifikia.
“Baada ya kuambiwa hivyo, kijana aliyekuwa na mategemeo ya kufunga ndoa na mrembo huyo, alimpeleleza mpenzi wake na kubaini mahali ambako kijana kutoka Marekani alifikia.
“Siku iliyofuata alivamia kwenye
 ile hoteli, akamkuta mpenzi wake na yule kijana wa Facebook, hapo 
ugomvi mkubwa ulizuka. Ugomvi haukuishia hapo kwa sababu kijana wa 
Nigeria aliahidi ni lazima aue mtu.
“Siku moja baada ya ugomvi 
hotelini, kijana wa Nigeria alimteka mpenzi wake na kumuua kwa 
kumkatakata na silaha inayodhaniwa kuwa ni panga,” alisema mtoa habari 
huyo.
Kwa mujibu wa mtandao huo mpaka pale habari hiyo inachapishwa, mtuhumiwa wa mauaji alikuwa hajakamatwa.
 
 
No comments:
Post a Comment